Dodoma FM
4 August 2026, 17:01

Dickson Dede Mwenyekiti wa Kijiji Cha Mguba amesema kuwa changamoto ya umbali imekuwa chanzo cha utoro Kwa wanafunzi licha ya kuendelea kuhamasisha jamii kujitolea ujenzi wa sekondari itakayo ondoa kadhia hiyo ya utoro.
Na Victor Chigwada.
Imeelezwa mshikamano iliyopo baina ya walimu na wazazi wa Kijiji cha Mguba imekuwa njia urahisi ya kupunguza wimbi la utoro wa rejereja kwa wanafunzi wa sekondari licha ya kutembea umbali mrefu
Wamesema Moja ya sababu za utoro ni wanafunzi kutumia muda mwingi kutembea mpaka kufikia shule ilipo Kata ya Iringa Mvumi
Lakini walimu na wazazi wamejitahidi kuhamasisha umuhimu wa watoto kwenda shuleni na kupunguza namba ya utoro shuleni