

10 October 2024, 7:00 pm
Na Steven Noel .
Migogoro imetajwa kuwa ni chanzo kikuu cha kuvunjika kwa mahusiano ya ndoa katika jamii kwa sasa.
Bi. Ruth Udamo Afisa Ustawi anayeshughulikia masuala ya usuluhishi wa migogoro ya ndoa Wilaya ya Mpwpwa anabainisha sababu kadhaa zinazopelekea kuwepo kwa migogoro mingi ya ndoa katika jamii.
Aidha Mchungaji wa Kanisa la Anglikana Mpwapwa mjini, Canon Habel Chitema amesema kuwa moja ya sababu ya kuwepo kwa migogoro ya ndoa ni pamoja na kijana kutaka kutimiza mahitaji yake ya kimwili.
Kwa upande wa wananchi wanaeleza kwamba uelewa mdogo wa jamii kuhusu dhana nzima ya ndoa ni mdogo hivyo kunasababisha kuwepo kwa ongezeko kubwa la talaka.