Dodoma FM

Wazazi watakiwa kuacha kushawishi wanafunzi kujifelisha

20 May 2025, 1:36 pm

Picha ni Baadhi ya wanafunzi wakipatiwa vifaa ikiwemo sare za shule ambapo ni msaada uliotolewa kwa wanafunzi  105 kutoka Shule saba katika kata ya Kibaigwa wilaya kongwa.Picha na Seleman Kodima.

Zaidi ya Watoto 450 wilayani kongwa wanapita changamoto ya ukosefu wa mahitaji muhimu

Na Seleman Kodima.

Mkuu wa Wilaya ya Kongwa Mayeka Saimon amewataka wazazi na walezi wilayani humo kuacha tabia ya kuwaambia watoto wao wafeli  mitihani ili kuwakatisha masomo  huku sababu ikiwa ni kushindwa kuwahudumia mahitaji ya shuleni ikiwamo Sare za Shule.

Kauli hiyo ameitoa wakati wa kukabidhi Msaada wa Sare za Shule na mahitaji mengine ya kujifunzia kwa wanafunzi  105 kutoka Shule saba katika kata ya Kibaigwa wilaya kongwa ambapo Msaada huo umetolewa na Mamlaka ya majisafi na usafi wa mazingira  Dodoma DUWASA kwa kushirikiana na Shirika la Dutcha water Operator( VEI).

Sauti ya Mayeka Saimon

Awali akielezea kuhusu msaada huo Mwakilishi wa Mkurugenzi mtendaji wa Mamlaka ya maji na Usafi wa mazingira Dodoma Bi Rahel Muhando amesema Mamlaka hiyo wanatambua umuhimu wa kushirikiana na  jamii .

Sauti ya Bi Rahel Muhando.
Picha ni Mkuu wa Wilaya ya Kongwa Mayeka Saimon akiongea wakati wa utoaji wa vifaa hivyo.Picha na Seleman Kodima.

Kwa upande wake Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Kongwa Mwl Master Mwashala ,sambamba na Mwakilishi wa walimu wakuu wa Shule saba ambazo wanafunzi wake wamepata msaada Loishooki Mollel  wameziomba taasisi nyingine kuwatazama watoto hao ili kuwawesha kupata mahitaji muhimu.

Sauti za Mwl Master Mwashala na Loishooki Mollel .

Pamoja na hayo inaelezwa kuwa zaidi ya Watoto 450 wilayani kongwa wanapita changamoto ya ukosefu wa mahitaji muhimu hivyo hatua ya Mamlaka ya maji na Usafi wa mazingira Dodoma  na VEI kutoa msaada kwa watoto 105 ni Nuru kwa Kundi hilo katika kufanikisha upatikanaji wa Elimu Bila Vikwazo.