Dodoma FM

Shinikizo la marafiki latajwa kuharibu vijana wengi

23 April 2025, 6:28 pm

Aina ya marafiki inaweza kuwa chachu ya mandeleo au chachu ya kukurudisha nyuma kutokana na ushauri wanaoutoa kwako.Picha na Google.

Sanjari na hayo wazazi wamewataka vijana kuzingatia malezi na maadili yanayofundishwa na wazazi wao, na kuongeza kuwa hakuna mzazi anayefurahia kuona mtoto wake anaharibikiwa.

Imeelezwa kuwa katika jamii, vijana wanakabiliwa na shinikizo kubwa kutoka kwa marafiki, jambo ambalo linaweza kuathiri maamuzi yao katika maisha.

Wakizungumza na Taswira ya habari baadhi ya vijana kutoka eneo la majengo jijini Dodoma wamesema kuwa aina ya marafiki inaweza kuwa chachu ya mandeleo au chachu ya kukurudisha nyuma kutokana na ushauri wanaoutoa kwako.

Sauti za vijana

Nao baadhi ya wazazi wamesema ni muhimu kwa vijana kufanya uchaguzi mzuri wa marafiki ili kujifunza mienendo na tabia nzuri kutoka kwao.\par

Sauti za wazazi