Dodoma FM
2 June 2026, 17:28

Elizabeth na Deogratias ni waumini wa kanisa Hilo wamesema wazazi na walezi wa Sasa wanejikita Katika utafutaji na kusahau jukumu la malezi na kuwaachia jukumu hilo wadada wa kazi.
Na Steven Noel.
Askofu msaidizi wa kanisa katoliki Jimbo kuu la Dodoma Mhasham Askofu Wilbroad Kibozi ameitaka Jamii kujikita Katika malezi yanayoendana na hofu ya Mungu Ili kuwa na taifa lenye tija.
Askofu Kibozi ameyasema hayo Katika parokia ya Bikra Maria wa Fatima Mpwapwa alipokuwa akizungumza katika Misa ya Kipaimara.
Amesema ili kuwa na kizazi chenye tija na hofu ya Mungu ni lazima wazazi na walezi kujikita Katika malezi yenye hofu ya Mungu.