Dodoma FM

Mwanafunzi abakwa na kuuawa kisha kutupwa shambani

5 May 2025, 18:14

Wakazi wa eneo hilo wakiwa wamekusanyika pamoja katika mkutano wa kijiji .Picha na Kitana Hamis.

Wakazi wa kijiji hicho wameiomba serikali iwasaidie ujenzi wa bweni ili kuwanusuru watoto na vitendo hivyo vya ukatili.

Na Kitana Hamis.

Suzana Samweli Mwenye umri wa Miaka 13  Mwanafunzi wa Darasa la Sita   amefariki Dunia Baada ya  kubakwa  na Kuuwawa Kisha kutobolewa Macho. katika Kijiji cha Gedamara kata ya Galapo wilayani Babati mkoani Manyara.

Tukio hilo limetokea April 29 ambapo baada ya tukio hilo mwili wa binti huyo ulitupwa katika shamba la mbaazi.

Wakazi wa kijiji hicho wameiomba serikali iwasaidie ujenzi wa bweni ili kuwanusuru watoto na vitendo hivyo vya ukatili

Kamanda wa polis mkoa wa Manyara Ahemd Makarani amethibitisha kutokea kwa tukio hilo ambapo amekiri kuwa mtuhumiwa anashikiliwa na jeshi la polisi huku uchunguzi mwingine ukiendelea.

Habari kamili.