Dodoma FM

Wanafunzi watakiwa kuto fumbia macho vitendo vya ukatili

18 August 2026, 16:53

Picha ni Jeshi la Polisi wilaya ya Mpwapwa kitengo cha dawati la jinsia wakati wakitoa Elimu ya ukatili Katika shule ya sekondari Mpwapwa.Picha na Stephen Noel.

Mpwapwa sekondari ni miongoni mwa shule inayojunuisha Wanafunzi kutoka mikoa mbalimbali  na shule ya bweni ambayo pia ni shule ya jumuishi.

Na Stephen Noel.

Jeshi la Polisi wilaya ya Mpwapwa kitengo cha dawati la jinsia  limewataka Wanafunzi wa shule za sekondari kuto nyamazia vitendo vya ukatili vinavyotokea Katika  Maeneo Yao Bali wayatolee taarifa Ili yaweza kuyathibitiwa.

Wakitoa Elimu ya ukatili Katika shule ya sekondari Mpwapwa Askari hao wamesema sehemu nyingi za mikosanyiko  ndio sehemu ambazo zinaweza weza kuwa vyanzo vya ukatili  hivyo wasisite kutoa taarifa ya vitendo hivyo.

Baadhi ya Wanafunzi wamesema aina ya ukatili unaweza kutoka Katika Maeneo ya shule ni ukatili wa kingono,ukatili wa kimwili,ukatili wa kisaikolojia na ukatili wa kiuchumi.

Sauti ya Noel.