Dodoma FM
Dodoma FM
7 May 2026, 16:22

Kwa sasa mkoa wa Dodoma upo vizuri kitaaluma ambapo mwaka uliopita ulishika nafasi ya pili.
Na Anwary Shaban.
Walimu wametakiwa kufuata kanuni na taratibu za utoaji adhabu shuleni ili kupunguza wimbi la utoro kwa wanafanzi.
Hayo yamesemwa na waziri wa nchi ofisi ya waziri mkuu Tamisemi Prof. Riziki Shemdoe alipo kuwa akizungumza katika mkutano wa wadau wa elimu uliofanyika jijini Dodoma mei 6 2026 amewataka walimu kuzingatia umri sahihi wa wanafunzi pindi wanapo toa adhabu shuleni.
Aidha amempongeza mkuu wa mkoa wa Dodoma Mhe ,Rosemery Senyamule kwa kuwapeleka walimu walio fanya vizuri kwenda kujifunza mafunzo nje ya nchi akiwa jumuisha walimu 34 na Mafisa Elimu 2 walio kwenda korea kujifunza zaidi.

Kwa upande wake mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe,Rosemery Senyamule amesema kwa sasa mkoa wa Dodoma upo vizuri kitaaluma ambapo mwaka uliopita ulishika nafasi yapili huku dhamira ya dhati ya mkoa ni kushika nafasi yakwanza kitaifa.
Nae Mkuu wa wilaya ya Dodoma Alhaj Jabir Shekimweri amempongeza Rais Samia Suluhu Hassan kwa mafanikio makubwa ambayo Tanzania imeendelea kuyapiga katika kukuza sekta ya elimu na kujiandaa kwa 2028 ambapo darasa la 6 na7 watahitimu kwa pamoja.