Dodoma FM

Vijana watakiwa kuchangamkia fursa mbalimbali kujiingizia kipato

28 April 2026, 15:33

Vijana wamesema vijana wengi wanatumia muda mwingi kwenye mitandao ya kijamii pasipo kubuni njia za kujiingizia kipato.Picha na Mtandao.

Serikali imeendelea kuboresha mazingira  ya kilimo  kwa kuweka mindombinu ya kisasa hususani katika kilimo cha umwagililiaji.

Na Victor Chigwada.

Vijana wametakiwa kujikita kwenye fursa mbalimbali ili kujiingizia kipato na kuacha kisingizio cha kukosa ajira .

Wakiongea na taswira ya habari  baadhi  ya vijana wamesema vijana wengi wanatumia muda mwingi kwenye mitandao ya kijamii pasipo kubuni njia za kujiingizia kipato au kuitumia mitandao hiyohiyo ya kijamii kujiingizia kipato.

Sauti vijana.

Ngw’ashi Muhuri afisa maendeleo Kata ya Msamalo amesema kuwa dhana potofu ya vijana kuamini watu wa vijijini ndio wanahusika na kilimo ndio imewafanya vijana wengi kuendelea kulalamikia ukosefu wa ajira .

Aidha amesema  Serikali imeendelea kuboresha mazingira  ya kilimo  kwa kuweka mindombinu ya kisasa hususani katika kilimo cha umwagililiaji hivyo vijana wanapaswa kuiona fursa ya kilimo na kuitumia kujikwamua kimaisha.

Sauti Mhuri