Dodoma FM

Utumaji wa nyaraka, usafirishaji vifurushi posta ni salama zaidi

10 October 2024, 3:28 pm

Na Anwary Shabani                                                             

Utumaji wa nyaraka na usafirishaji wa vivurushi kupitia Shirika la Posta ni salama zaidi kulinganisha na njia zingine.

Wadau na watumiaji wa huduma za Posta wamebainisha hayo wakati wa hafla ya kukabidhi zawadi kwa watumiaji bora wa huduma za posta pamoja na washindi wa shindano la uandishi katika kuadhimisha siku ya posta duniani na wiki ya huduma kwa mteja.

Pichani mdau wa huduma za posta akieleza ubora wa huduma za shisrika la posta
Sauti ya mdau

Katika maadhimisho hayo, Elton Thomson ambaye ni mwanafunzi ameibuka mshindi kwa kujishindia kitita cha pesa taslim kiasi cha Tsh 700,000/= (shilingi laki saba) katika shindano la uandishi .

Elton Thomson mshindi wa shindano la uandishi posta
Sauti ya Elton Thomson

Ufanisi wa utoaji wa huduma kwa shirika la posta kunatokana na  jitihada za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuliwezesha shirika hilo kujiendesha na kutengeneza faida. Meneja wa shirika la posta Dodoma Bwn. Dongwe James Dongwe amepongeza na kushukuru kwa jitihada hizo.

Pichani meneja wa shirikala posta Bwn, Dongwe James Dongwe.
Sauti ya Bwn. Dongwe James Dongwe.