Dodoma FM

Marufuku kuingiza, kusafirisha nguruwe Mpwapwa

27 April 2026, 15:17

Wakulima wengi wamepata hasara kutokana na wanyama wao kufa. Picha na Kilimo hai.

Amesema wamefikia hatua hiyo kutokana na ugonjwa wa nguruwe  unaosababishwa na virusi na hauna tiba wala kinga .

Na Steven Noel.

Kaimu Afisa Mifugo  Wilaya ya Mpwapwa mkoani Dodoma Dkt. Emanuel Lyimo amesema kufuatia kuwepo wa ugonjwa wa nguruwe kwa baadhi ya maeneo katika wilaya ya Mpwapwa wamepiga marufuku kuingiza au kusafirisha  nyama, mnyama au aina yoyote ya bidhaa zitokanazo na mnyama huyo  kwa lengo la kudhibiti ugonjwa.

Dkt Lyimo amesema  wakulima wengi wamepata hasara  kutokana na wanyama wao kufa.

Wakiongea na Taswira ya Habari, baadhi ya wananchi wilayani Mpwapwa wameiomba serikali kufanya utafiti ili kuzuia ugonjwa huo kwani unapelekea wafugaji kupata hasara.

Sauti ya kina