Dodoma FM
12 June 2026, 13:24

Aina fulani za magonjwa ya zinaa yanaweza kuambukizwa kutoka kwa mama hadi kwa mtoto.
Na Mariam Kasawa.
Kwa mujibu wa Shirika la Afya Duniani (WHO), zaidi ya watu milioni moja duniani kote wanaambukizwa magonjwa ya zinaa kila siku.
Magonjwa kutosikia matibabu ni tatizo kubwa la magonjwa ya zinaa (STDs) au (maambukizi ya zinaa) na ni kikwazo kikubwa katika kudhibiti magonjwa ya zinaa, WHO ilisema.
Kulingana na WHO, magonjwa ya zinaa huathiri uwezo wa kujamiiana na uzazi, na huongeza hatari ya ugumba, matatizo ya ujauzito, saratani na VVU/UKIMWI.
Zaidi ya bakteria 30, virusi na vimelea (fangasi) huambukizwa kutoka kwa mtu mmoja hadi kwa mwingine kupitia ngono ya uke, njia ya haja kubwa na ya mdomo.