Dodoma FM

Wafanyabiashara wa kokoto waomba bei elekezi

8 August 2023, 4:46 pm

Wafanyabiashara hao wanalalamika kuto kuwa na bei elekezi katika biashara hiyo hali inayo pelekea kila mtu kuuza kwa bei yake. Picha na Facebook.

Ni muhimu kuwepo kwa upangaji na usimamizi wa bei elekezi katika shughuli mbalimbali za kibiashara, ili kuepusha migongano kati ya wafanyabiashara kutokana na kujipangia bei zao wenyewe na ushawishi binafsi kutoka kwa wateja.

Na Neema Shirima.

Baadhi ya Wafanyabiashara wa kokoto Jijini Dodoma wametoa pendekezo la kuwepo kwa umoja na  usimamizi wa bei elekezi katika biashara hiyo, hii ni kwa sababu baadhi ya wafanyabiashara hao kukosa ushirikiano na kupanga bei zao wenyewe.

Akizungumza na Taswira ya Habari Bw. Mohamed Ramadhani mmoja wa wafanya biashara hao katika eneo la Mailimbili Darajani ametoa wito na kuwaomba  wafanyabiashara wenzake kuwa na umoja katika shughuli hiyo na kuuza kwa bei elekezi bila kuangalia ushawishi wa wateja kwa wote wanaitegemea shughuli hiyo kujipatia kipato.

Sauti ya mfanyabiashara wa Kokoto

                                      

Wauzaji hao wanaomba kuwepo vikao vya wafanyabiashara hao ili wakubaliane bei moja. Picha na facebook.

Aidha Bw. Isa Zuberi ambaye ni miongoni wamfanyabiashara katika eneo hilo amesema kuwa, sababu kubwa ya wafanyabiashara hao kutofautiana bei katika uuzaji wa kokoto, ni makubaliano binafsi kati ya mteja na mfanyabiaShara husika anayefikiwa na mteja licha ya kukiri kuwa bei waliyo kubaliana kuitumia katika eneo hilo ni Shilingi 2500 kwa ndoo moja huku akitoa ombi la kuwepo kwa vikao kati yao.

Sauti ya Bw Zuberi muuzaji wa Kokoto.

Kwa upande wake mmoja wa  watengenezaji wa kokoto hizo Bw. Abdalah Issa amesema kuwa, kwao hali ni tofauti kwani malipo yao hufanyika kwa siku pale tu wanapo maliza shughuli ya kuponda kokoto kwa kiwango walicho kubaliana na mwajiri wake.

Sauti ya mtengenezaji wa kokoto.