Dodoma FM

Uzalishaji wa maji Nzuguni waongeza asilimia 11.7 ya maji

27 March 2024, 5:10 pm

Picha na Mhandisi wa maji Duwasa James Rioba akiongea na Mulika ya Dodoma Tv.Picha na George John.

Mradi wa Maji Nzuguni umegharimu bilion 4.3 lengo likiwa ni kuboresha huduma ya usambazaji maji katika kata na jiji la Dodoma kwa ujumla.

Na Mindi Joseph.
Kukamilika kwa Mradi wa awamu ya kwanza wa Visima 5 vya maji Eneo la nzuguni umeongeza asilimia 11 .7 ya maji yanazalishwa kutoka lita 68,600,000 hadi 76,000,000 kwasiku.

Visima 5 vya mradi huo vinahudumia wananchi elfu 75000 huku visima vitano vya awamu ya pili vikitarajia kuhudumia maeneo ya kisasa,nyumba 300 na maeneo mengine.

Mhandisi wa maji Duwasa James Rioba anasema mradi huu wa maji ndio mkubwa kwa mwaka huu wa fedha.

Sauti ya Mhandisi wa maji Duwasa James Rioba.
Picha ni sehemu ya kutunzia dawa kwaajili ya kutibu maji .Picha na George John.

Miongoni mwa wananchi wamepongeza mradi huo kwa kuwatatulia changamoto ya maji.

Sauti za wananchi.

Mwenyekiti wa mtaa wa Nzunguni A Onaely Mbatiani anasema Mradi wa maji nzuguni umemaliza changamoto ya maji kwa wananchi wake.

Sauti ya Mwenyekiti wa mtaa wa Nzunguni A Onaely Mbatiani .