Dodoma FM

Kausha damu chanzo cha migogoro ya ndoa Mpwapwa

12 May 2026, 16:36

Picha ni wasaidizi wa msaada wa kisheria wakiwasaidia wananchi wilayani Mpwapwa.Picha na Steven Noel.

Aidha ametoa wito Kwa Wananchi  kuzingatia taratibu za kisheria  Ili kupunguza migogoro au kuepuka kuingia Katika makosa ya jinai.

Na Stephen Noel .

Wananchi wa wilaya ya Mpwapwa wamejitokeza kupata msaada wa kisheria unaotolewa na timu ya  mama Samia Legal Aid Katika viwanja mashujaa .

Wakiongea na Taswira ya habari wananchi hao wamesema watu wengi wanakabiliwa na changamoto ya migogoro ya ndoa ,Ardhi na mirathi hivyo kusogezewa huduma ya msaada wa kisheria karibu itawasaidia kutatua kero hizo.

Aidha baadhi ya wanawake wamesema migogoro mingi ya ndoa katika eneo hilo inatokana na wanawake kujiingiza katika mikopo umiza maarufu kama kausha damu bila kuwashirikisha wenza wao na kujikuta wakipoteza vitu.

Jene mbelwa mmoja wa wanasheria katika walipo katika eneo hilo la Mpwapwa amesema  uelewa mdogo wa Sheria Kwa Wananchi hupelekea baadhi kupoteza Haki zao za Msingi .

Sauti ya Kina Noel.