Dodoma FM
Dodoma FM
2 April 2026, 17:25

Mwaka 2022 serikali ilitoa waraka wa wananafunzi wa kike wanaopata ujauzito kurejea mara baada ya kujifungua .
Na Steven Noel.
Wadau wa Elimu Katika kata nne za wilaya ya Mpwapwa wamesema bado mkakati uliotolewa na serikali wa kuwarejesha shule wanafunzi waliopata ujauzito bado haueleweki kwa jamii.
Wakijadili kwenye kikao cha siku mbili kilichodhaminiwa na shirika la Haki Elimu wadau wa elimu kutoka kata za Mazae,Mpwapwa mjini ,Godegode na Pwaga wamesema pamoja na serikali kutoa waraka huo wa mwaka 2022 lakini bado uelewa wa jamii ni mdogo juu ya kuwarejesha shuleni mabinti hao.
Aidha wamesema sababu zingine ni pamoja na mlolongo mrefu wa ufuatiliaji wa urejeaji shule ambao unasababisha baadhi ya wazazi kukata tamaa.
Kwa upande wake Afisa kutoka shirika la Haki Elimu Dkt ,Wilbafoce Meena amesema tafiti zilizofanywa na shirika lake zimebaini uelewa mdogo wa jamii,unyanyapaa uliopo kwa baadhi ya walimu na wanafunzi kwa mabinti waliopata ujauzito nazo ni sababu zinazopelekea wengi kushidwa kurudi.