Dodoma FM

Soko la Kariakoo ni mchango mkubwa kwa uchumi wa taifa

19 June 2025, 4:55 pm

Jumla ya wafanyabiashara 30 wa kariakoo ambao ni washindi wa Tuzo za kariakoo wamewasili leo Jijini Dodoma.Picha na Mtanzania.

Jumla ya wafanyabiashara 30 wa kariakoo ambao ni washindi wa Tuzo za kariakoo wamewasili leo Jijini Dodoma baada ya kupokea mwaliko wa kushiriki vikao vya bunge na watatembelea Miradi mbalimbali katika Jiji la  Dodoma.

Na Seleman Kodima.

Wafayabiashara wa Soko la Kariakoo wametajwa kuwa na Mchango mkubwa katika maendeleo ya uchumi wa  Taifa.

Nchini Tanzania   soko kubwa na  linalofanya vizuri ni Kariakoo lakini kwa sehemu kubwa wafanyabiashara hawa wanasahaulika kwenye eneo la kupongezwa na kwa jitihada wanazozifanya.

Akizungumza na waandishi wa habari leo June 19 baada ya kuwasili Dodoma Mwazilishi Wa Tuzo za Wafanyanbiashara Kariakoo  Zakayo Shushu  anasema lengo  la Tuzo hizi ni kusaidia wafanyabiashara kutambulika kwa jamii na kutambua mchango wao katika uchumi wao.

Sauti ya Zakayo Shushu.

Baadhi ya wafanyabiashara wanasema hii imekuwa ni fursa ya kipee ya kuwapa hamasa pamoja na kuamika kwa jamii huku wakiomba marekebisho ya wafanyabiashara wageni kuingilia biashara za wafanyabiashara wa Ndani.

Sauti za wafanyabiashara.

Cornel Kyai Ni afisa mwandamizi Shirika la Reli Tanzania amewakarishisha wafanyabiashara kufanya biashara zao katika Jengo la Stesheni.

Sauti ya Cornel Kyai .