Dodoma FM

Wazazi watakiwa kuendelea kuwalinda watoto dhidi ya mitandao

14 May 2026, 16:38

kusambaza picha au video ya mtoto akiwa uchi, mazingira ya fedheha, kuchapisha taarifa binafsi  za  mtoto zinazoweza kuhatarisha maisha yake.Picha na Mtandao.

Vile  vile kupitia sheria ya mtoto kifungu cha 9 kinaeleza wajibu wa mzazi au mlezi kumlinda mtoto dhidi ya ukatili,udhalilishaji na mazingira yanayoweza kumdhuru.

Na Jerome John.

Wazazi na walezi mkoani Dodoma wamekumbushwa kuendelea kuwalinda watoto wao dhidi ya matumizi yasiofaa ya mitandao ya kijamii.

Kwa mujibu wa sheria ya mtoto wazazi,walezi na jamii kwa ujumla wana wajibu wa kumlinda mtoto kwenye mazingira ya kidigitali yasiweze kumuathiri.

Kupitia  sheria  hiyo Mkaguzi msaidizi  wa jeshi la polisi na afisa dawati la jinsia na Watoto Dodoma  Michael Mkinda ameitaka jamii kwa ujumla kuzingatia matumizi  ya  mitandao ya kijamii wanayo itumia bila kuwaathiri watoto.

Sauti ya  Michael Mkinda.

Aidha amesisitiza kuwa kusambaza picha au video ya mtoto akiwa uchi, mazingira ya fedheha, kuchapisha taarifa binafsi  za  mtoto zinazoweza kuhatarisha maisha yake  Pamoja na kumrekodi akiadhibiwa ni kosa kwa mujibu wa sheria kifungu cha 158(1)(a) na (c).