Dodoma FM

Miradi 6 yenye thamani Bilion  1.6  yazinduliwa na mbio za mwenge Mpwapwa

1 June 2026, 17:20

Picha ni Mkuu wa wilaya ya Mpwapwa mh. Sophia Kizigo akipokea mwenge wa uhuru wilayani humo.Picha na Mpwapwa District.

Mbio za mwenge wa uhuru mwaka 2026 zinabebwa na kaulimbiu isemayo Tanzania ni yetu sote tushikamane  Kwa pamoja kuleta maendeleo.

Na Steven Noel.

Jumla ya miradi sita yenye thamani ya shilingi  Bilion 1.6 imezinduliwa kutembelea na kuwekewa mawe ya Msingi na mwenge wa uhuru  Kwa mwaka 2026 wilayani Mpwapwa.

Kiongozi wa mbio za mwenge mwaka 2026 Bwana Wazo Michael Mwang’onda  amewataka watendaji wote wa serikali  kutanguliza uzalendo mbele Ili miradi inayotolewa na serikali iweze kuwa na faida Kwa Wananchi wote .

Aidha ametumia fursa hiyo kuwahamasisha Wananchi wote kuweza kuendelea ,kulinda  Amani ya Taifa kwa kuto kujihusisha kwenye vitendo vyovyote vinavyoweza kusababisha uvunjivu wa Amani.

Kwa upande wake Mkuu wa wilaya ya Mpwapwa Dkt Sophia Mfaume Kizigo amesema  miradi hiyo iliyotembelewa na  mbio za mwenge itakuwa chachu ya maendeleo Kwa wilaya  hiyo Kwa mtu mmoja mmoja na Jamii Kwa jumla.

Sauti ya Kina Noel.