Dodoma FM

Waziri Kapinga aipongeza Mainland kwa uwekezaji mkubwa

26 June 2026, 12:48

Picha ni waziri wa viwanda na biashara mh.Judith Kapinga alipotembelea katika kiwanda hicho .Picha na Mariam.

Serikali imeendelea kuchukua hatua mbalimbali ikiwemo maboresho ya sera, sheria na mifumo ya kodi ili kuvutia uwekezaji zaidi katika viwanda vya mafuta ya kula na kuongeza uzalishaji wa ndani.

Na Mariam Kasawa.
Serikali imeahidi kuendelea kuweka mazingira bora kwa wawekezaji katika sekta ya viwanda ili kuchochea ukuaji wa uchumi hapa Nchini.

Hayo yamesemwa na waziri wa viwanda na biashara mh.Judith Kapinga alipotembelea katika kiwanda cha kuchakata na kuzalisha mafuta ya kula Mainland kilichopo Veyula jijini Dodoma ambapo katika ziara hiyo waziri Kapinga amejionea shughuli mbalimbali zinazo fanyika kiwandani hapo.

Waziri Kapinga amesema viwanda vya kuongeza thamani ya mazao ya ndani vina nafasi muhimu katika kufanikisha malengo ya maendeleo ya Taifa pamoja na utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.

Sauti ya mh.Judith Kapinga.
Picha ni waziri wa viwanda na biashara mh.Judith Kapinga akipokea zawadi kutoka kwa Mkurugenzi Mkuu wa kiwanda hicho, Bw. Jiaweli Chen, Pembeni ni mkurugezi wa Mawasiliano katika kiwanda hicho Bi Betty Mkwasa.Picha na Mariam .

Amesema Serikali imeanza kushirikiana na Wizara ya Kilimo pamoja na taasisi zake kuweka mikakati ya kuongeza uzalishaji wa mazao ya mafuta ili kuhakikisha viwanda vinapata malighafi za kutosha.

Sauti ya mh.Judith Kapinga.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa kiwanda hicho, Bw. Jiaweli Chen, ameishukuru Serikali kwa kuendelea kuboresha mazingira ya uwekezaji na kutoa ushirikiano unaowezesha viwanda kufanya kazi kwa ufanisi amesema hatua hiyo inaonesha utayari wa viongozi kushirikiana na sekta binafsi katika kutafuta suluhisho la changamoto zinazojitokeza wakati wa utekelezaji wa shughuli za uzalishaji.

Sauti ya Bw. Jiaweli Chen,

Akiongea mara baada ya kutamatika kwa ziara hiyo mkurugezi wa Mawasiliano katika kiwanda hicho cha Mainland Bi. Betty Mkwasa amemesema kiwanda hiki kimetoa fursa kubwa kwa vijana kupata ajira ambapo hadi sasa zaidi ya vijana 400 wameajiriwa katika kiwanda hicho .

Sauti ya Bi. Betty Mkwasa

Serikali imeendelea kuchukua hatua mbalimbali ikiwemo maboresho ya sera, sheria na mifumo ya kodi ili kuvutia uwekezaji zaidi katika viwanda vya mafuta ya kula na kuongeza uzalishaji wa ndani.