Dodoma FM

EFL Dodoma yachagiza kaulimbiu Dodoma ya kijani kwa kupanda miti

10 October 2024, 19:00

Na Mariam Kasawa.

Kampuni ya mikopo ya Enterprice Financial Limited EFL imechagiza kauli mbiu ya Dodoma ya Kijani kwa kupanda miti  katika maeneo ya Kndege Shule ya Msingi iliyopo jijini Dodoma.

Meneja wa ampuni hiyo ya EFL tawi la Dodoma Bwn. Niwakoel Ndosa amesema wameamua kuunga mkono kaulimbiu ya Dodoma ya Kijani kwa kupanda miti katika Shule ya Msingi K ndege ikiwa ni sehemu ya kurejesha kwa jamii.

Meneja wa ampuni ya EFL tawi la Dodoma Bwn. Niwakoel Ndosa
Sauti ya Bwn. Niwakoel Ndosa

Muhifadhi Mkuu kutoka wakala wa misitu Tanzania TFS Bi. Husna Msagati amesema miti hiyo inapaswa kutunzwa ili kutimiza kauli mbiu ya Dodoma ya kijani.

Muhifadhi Mkuu kutoka wakala wa misitu Tanzania TFS Bi. Husna Msagati
Sauti ya Bi. Husna Msagati

Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Kndege amesema amefurahishwa na zoezi hilo la upandaji miti kwani limesaidia wanafunzi kushiriki kwa vitendo elimu ya utunzaji mazingira.

Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Kndege
Sauti ya Mwalimu Mkuu Kndege S/M

Zoezi hilo la upandaji miti lililofanyika shuleni hapo mapema leo hii limehudhuriwa na wadau mbalimbali wakiwemo wakala wa misitu Tanzania TFS, NEMC, mwenyekiti wa mtaa , Diwani wa Kata ya Kndege. pamoja na wanafunzi.

Pichani moja ya nwanafunzi akieleza jinsi watakavyotunza miti iliyopandwa na TFL
Sauti ya mwanafunzi Kndege S/M