Nani anaathirika zaidi na mabadiliko ya tabianchi?
3 September 2026, 16:56

Makubaliano ya mjini Paris mwaka 2015 yaliweka kipaumbele maalum cha kuwawezesha na kutambua kwamba wanawake huathiriwa kwa kiasi kikubwa zaidi katika jamii kutokana na mabadiliko ya tabia nchi.
Na Mariam.
Miaka kumi baada ya Mkataba wa Paris, utoaji wa gesi chafuzi zinazochangia ongezeko la joto duniani unaendelea kuongezeka, na mwaka jana mabadiliko ya joto duniani kwa mwaka yalivuka nyuzi joto 1.5 kwa mara ya kwanza.
Hata hivyo, bado inawezekana kufikia lengo la nyuzi joto 1.5, na wataalamu hao wawili wamebainisha majawabu mbalimbali, ikiwemo kuhama kutoka kwa nishati ya mafuta ya kisukuku hadi vyanzo safi vya nishati, pamoja na kubadilisha mifumo ya chakula ili kuondoa upotevu.
Tafiti zinaonyesha kuwa wanawake wana uwezekano mkubwa kuathirika na mabadiliko ya tabia nchi zaidi ya wanaume.
Kwa mujibu wa takwimu za Umoja wa Mataifa asilimia 80 ya watu wanaolazimika kuhama makazi yao kutokana na mabadiliko ya tabia nchi ni wanawake.
Majukumu yao kama walezi na wanao hudumia familia kwa karibu zaidi huwafanya kuwa katika mazingira hatari zaidi wakati wa mafuriko na ukame unapotokea.