Dodoma FM
3 September 2026, 16:34

Baadhi ya wazazi wamesema tangu kuanzishwa kwa utaratibu wa chakula shuleni kumekuwa na mabadiliko ya taaluma kwa watoto wao kupelekea hamasa kwa wazazi ambao walikuwa hawana mwamko wa kuchangia chakula shuleni.
Na Victor Chigwada.
Juhudi za wazazi wa kijiji cha makang’wa za kuhakikisha watoto wanapata chakula shuleni umeleta matokeo chanya kwa kuongeza kiwango cha ufaulu kwa wanafunzi.
Akiongea na taswira ya habari mwenyekiti wa kijiji cha makang’wa bw.aidani mamba amesema mchakato huo wa chakula umepelekea kupunguza utoro shuleni na kupelekea wanafunzi wa shule hiyo kuwa na ari ya kusoma.