Dodoma FM
Dodoma FM
20 March 2026, 16:45

Gari hiyo ambayo ilikuwa ikiendeshwa kwa mwendo kasi iliacha njia ghafla na kuvamia makazi ya watu.
Na Steven Noel
Watu watatu wamenusurika kufa katika ajali baada ya gari aina ya lori lenye usajili namba T676DFC lililobeba kokoto kuacha njia na kugonga makazi ya watu katika mtaa wa Hazina namba 30 wilayani Mpwapwa.
Wakiongea na Taswira ya Habari, mashuhuda wa ajali hiyo wamesema gari hiyo ambayo ilikuwa ikiendeshwa kwa mwendo kasi iliacha njia ghafla na kuvamia makazi ya watu yaliyo karibu na barabara hiyo.
Akithibitisha kutokea kwa ajali hiyo diwani wa kata ya hazina Bw.Emanuel Ndule amesema watu watatu wamejeruhiwa katika ajali hiyo na tayari wamepelekwa hospitali kwaajili ya matibabu.