Dodoma FM

Ujenzi wa sekondari Mapinduzi wapunguza adha ya wanafunzi kutembea umbali mrefu

26/02/2026, 11:57

Uwepo wa shule hiyo ya sekondari umepunguza gharama za wazazi kuwapangishia watoa wao vyumba.Picha na Mtandao.

Wananchi wa eneo hilo wameishukuru serikali kwa kutoa fedha kwaajili ya ujenzi wa sekondari hiyo.

Na Victor Chigwada.

Ujenzi wa shule ya sekondari Mapinduzi A umekuwa mkombozi Kwa wanafunzi wa mtaa huo ambao hapo awali walilazimika kutembea umbali mrefu hadi shule ya sekondari  Ngh’ongh’ona .

Baadhi ya wazazi walilazimika kuwapangia vyumba watoto wao karibu na shule hali iliyo hatarisha usalama hasa kwa watoto wa kike .

Sauti za wananchi

Golden Mathayo mwenyekiti wa mtaa wa Mapinduzi A ameishukuru Serikali Kwa kutoa fedha za kujenga sekondari hiyo ambayo awali ilikuwa ni changamoto Kwa wanafunzi wa mtaa huo.

Mathayo ameongeza kuwa uwepo wa shule hiyo ya sekondari umepunguza gharama za wazazi kuwapangishia watoa wao vyumba lakini zaidi imekuwa ni fursa ya kuwalea watoto wao Kwa ukaribu zaidi.

Sauti ya Golden Mathayo.