Dodoma FM
Dodoma FM
13 Aprili 2026, 16:28

Kwa mwaka 2026 Kauli mbiu ya maadhimisho hayo ni malezi na ulinzi wa mtoto ni WAJIBU wetu sote.
Na Steven Noel.
Jamii imeshauriwa kuchukua hatua dhidi ongezeko la watoto wanaotumikishwa mitaani pamoja na ongezeko la watoto wa mitaani linalozidi kuongezeka siku hadi Siku.
Wito huo umetolewa na kaimu Mkuu wa wilaya ya Mpwapwa ambae ni katibu tarafa Mima Bi Arene Milinga kwenye kilele cha maadhimisho ya ya Siku ya kimataifa ya watoto wanaoishi na kufanya kazi mtaani ,
Amesema kuwa tafiti na taarifa mbalimbali zinadai migogoro ya ndoa pamoja umaskini wa kipato cha familia ni chanzo moja wapo cha watoto wanaotumikishwa mitaani .
Aidha Afisa ustawi wa halmashauri ya wilaya ya Mpwapwa Bi. Rose Sichilima amesema tangu maadhimisho hayo yaanze tarehe mosi Kwa wilaya ya Mpwapwa wamewabaini watoto 235 wakiwa wasichana 135 na wavulana 89 wanaotumikishwa kazi mbalimbali .

Naye Afisa maendeleo ya Jamii kitengo cha watoto Bwana Zakaria Kiondo amesema lengo la maadhimisho hayo ni kuikumbusha Jamii juu ya kuchukua hatua dhidi ya utoaji wa Haki za malezi Kwa watoto wanaoishi na kutumikishwa mitaani.