Dodoma FM

Ndogowe barabara yaharibiwa na mvua

8 April 2026, 11:35

Wamesema mvua za masika zilizonyesha mfululizo zimepelea barabara ya eneo hilo kuwa na mashimo. Picha na mtandao.

Changamoto ya miundombinu mibovu ya barabara imepelekea wagonjwa kushindwa kufika hospitali kwa wakati pamoja usafiri kuwa washida.

Na Victor Chigwada.

Wakazi wa Kijiji Cha Ndogowe wilayani Chamwino wameiomba Serikali kukarabati miundombinu ya barabara  zilizo haribiwa na mvua na kupelekea adha ya usafiri.

Wakiongea na Taswira ya habari wananchi hao wamesema mvua za masika zilizo nyesha mfululizo zimepeleakea barabara ya eneo hilo kuwa na mashimo pamoja na kutengeneza madimbwi ya maji hali inayokwamisha usafiri katika eneo hilo.

Aidha wamesema changamoto ya miundombinu mibovu ya barabara imepelekea wagonjwa kushindwa kufika hospitali kwa wakati pamoja usafiri kuwa washida.

Sauti za wananchi.

Keneth Muhawi mwenyekiti wa Kijiji hicho amekiri uwepo wa adha ya miundombinu ya barabara iliyochangiwa na mvua zilizo kuwa kikiendelea kunyesha

Sauti ya Bw.Keneth Muhawi.