Dodoma FM
Dodoma FM
19/03/2026, 16:02

Tume ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora itawalisha taarifa mbalimbali za utekelezaji wa majukumu ya tume, kujadili na kutolea maelekezo kwenye mkutano wake.
Na Anwary Shaban.
Tume ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora imepanga kujadili malalamiko mbalimbali yaliyowasilishwa na watumishi wa umma kuanzia Machi 23 Aprili 15 .
Hayo yamesemwa na kaimu katibu wa Tume hiyo John Mbisso jijini Dodoma wakati alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari ambapo ameeleza kuwa mkutano huo utalenga kujadili rufaa na malalamiko ya watumishi wa umma .
Aidha katika mkutano huo Tume itapitia taarifa mbalimbali za utekelezaji wa majukumu ya tume pamoja na kuwasilisha taarifa na kuzijadili.