Dodoma FM
Dodoma FM
27 February 2026, 17:03

Aidha amewahimiza wakazi wa Chinyika wajitokeze kwa wingi katika mkutano utakaofanyika kesho
Na Farashuu Abdallah.
Wakazi wa mtaa wa Chinyika kata ya Mkonze jijini Dodoma wameiomba serikali kutatua changamoto ya maji ambayo imekuwa ni kero ya muda mrefu.
Wakizungumza na Dodoma Fm baadhi ya wananchi hao wamesema changamoto hiyo ya maji imekuwepo tangu mwaka 2023 ambapo wamekuwa wakitegemea kisima kimoja huku wakiiomba Serikali iwatatulie changamoto hiyo.
Kwa upande wake mwenyekiti wa mtaa wa Chinyika Bw.Kombo Ally Kombo ametolea ufafanuzi changamoto hiyo ambapo amesema Serikali ipo kwenye mikakati ya kutatua changamoto hii.
Aidha amewahimiza wakazi wa Chinyika wajitokeze kwa wingi katika mkutano utakaofanyika kesho wenye lengo la kuzungumzia mustakabali wa changamoto hiyo.