Dodoma FM
Dodoma FM
19 February 2026, 4:24 pm

Viongozi wa eneo hilo wamelalamikiwa kushidwa kuwachukulia hatua wahusika wa uharibifu wa mazingira hayo.
Na Steven Noel.
WAKAZI WA Kitongoji cha Mcheula Kijiji cha Idilo kata ya Mazae wilaya ya Mpwapwa wamelalamikia matokeo ya uharibifu wa Mazingira Katika milima ya Idilo na Nguji kulima milimani huko wahusika kuto kuchukuliwa hatua .
Wakiongea na Taswira ya Dodoma Fm baadhi ya Wakazi wa Kitongoji hicho wamewalalamikia Viongozi waliopewa mamlaka kushidwa kuwachukulia hatua wahusika wa uharibifu wa mazingira hayo .
Ezely Chalio ni mwenyekiti wa Kitongoji cha Mcheula amekili kuwepo Kwa baadhi ya Wananchi mashamba Yao kusombwa na Maji na hivyo kuwasababishia hasara kubwa.