Dodoma FM

Wakazi wa Idilo walia na uharibifu wa mazingira

19 February 2026, 4:24 pm

Picha ni eneo uharibifu ulio fanywa na mvua katika eneo hilo.Picha na Steven Noel.

Viongozi wa eneo hilo wamelalamikiwa kushidwa kuwachukulia hatua wahusika wa uharibifu wa mazingira hayo.

Na Steven Noel.

WAKAZI WA Kitongoji cha Mcheula Kijiji cha Idilo kata ya Mazae wilaya ya Mpwapwa wamelalamikia matokeo ya uharibifu wa Mazingira  Katika milima ya Idilo na Nguji kulima milimani huko wahusika kuto kuchukuliwa hatua .

Wakiongea na Taswira ya Dodoma Fm  baadhi ya Wakazi wa Kitongoji hicho wamewalalamikia Viongozi waliopewa mamlaka kushidwa kuwachukulia hatua wahusika wa uharibifu wa mazingira hayo .

Ezely Chalio ni mwenyekiti  wa Kitongoji  cha Mcheula  amekili  kuwepo Kwa baadhi ya Wananchi mashamba Yao kusombwa na Maji na hivyo kuwasababishia  hasara kubwa.

Sauti ya kina.