Dodoma FM
Dodoma FM
19/02/2026, 16:24

Viongozi wa eneo hilo wamelalamikiwa kushindwa kuwachukulia hatua wahusika wa uharibifu wa mazingira hayo.
Na Steven Noel.
WAKAZI WA Kitongoji cha Mcheula Kijiji cha Idilo kata ya Mazae wilaya ya Mpwapwa mkoani Dodoma wamelalamikia matokeo ya uharibifu wa mazingira katika milima ya Idilo na Nguji kutokana na baadhi ya watu kuendesha kilimo katika milima hiyo bila kuchukuliwa hatua .
Wakiongea na Taswira ya Dodoma Fm baadhi ya wakazi wa Kitongoji hicho wamewalalamikia viongozi waliopewa mamlaka kushindwa kuwachukulia hatua wahusika wa uharibifu wa mazingira hayo .
Ezely Chalio, mwenyekiti wa Kitongoji cha Mcheula amekiri kuwepo Kwa baadhi ya wananchi ambao mashamba yao yamsombwa na maji na hivyo kuwasababishia hasara kubwa.