Dodoma FM
Dodoma FM
13 Aprili 2026, 11:46

Mikopo umiza imekuwa ikipelekea athari nyingi kwa jamii ikiwemo familia zinazo jiingiza kwenye mikopo hiyo kukumbwa na madeni yasiyo kwisha.
Na Victor Chigwada
Wakazi wa Kata ya Ngh’ambaku Wilayani Chamwino wametakiwa kuachana na mikopo umiza maarufu kama kausha damu kwani imekuwa ikiathiri maisha yao.
Akiongea na Taswira ya habari Afisa maendeleo wa Kata ya Ngh’ambaku Bw.Richad Kisubi amesema jamii bado inahitaji elimu ya kutosha juu ya mikopo ili kufahamu madhara ya mikopo umiza na kuchukua mikopo rafiki ikiwemo mkopo nafuu wa asilimia 10 unao tolewa na serikali.
Aidha amewataka wananchi kabla ya kuchukua mikopo hiyo ni vema kupitia Kwa makini masharti ya mtoa mkopo ili kuepuka upotevu wa mali na kufilisiwa baada ya kushindwa kurejesha mkopo huo.
Kisubi ameongeza kuwa mikopo umiza imekuwa ikipelekea athari nyingi kwa jamii ikiwemo familia zinazo jiingiza kwenye mikopo hiyo kukumbwa na madeni yasiyo kwisha na kupelekea ugumu wa maisha ulio kithiri.
Nao baadhi ya wananchi hususani kundi la akina mama ambalo ndilo limekuwa likiathirika zaidi na mikopo hiyo wameeleza ni kwanini wamekuwa wakiingia katika mikopo hiyo.