Dodoma FM

Wananchi Bwawani waombwa kuwa watulivu sakata la bomoa bomoa

23 February 2026, 3:47 pm

kinachosubiriwa kwa sasa ni mazungumzo baina ya viongozi wa mtaa na ofisi ya mkurugenzi.Picha na Mtandao.

Mwenyekiti wa mtaa wa Bwawani ameeleza hatua ambazo zinaendelea hadi sasa kuhusu ubomoaji huo.

Na Farashuu Abdallah.

Ikiwa ni miezi kadhaa imepita tangu  Wananchi wa Mtaa wa Bwawani kata ya Mkonze jijini Dodoma kutoa malalamiko yao kuhusu uamuzi uliochukuliwa na ofisi ya Mkurugenzi wa kubomoa nyumba zao bila taarifa yoyote, mwenyekiti wa mtaa huo ametolea ufafanuzi juu ya kinachoendelea mpaka sasa.

Akizungumza na Dodoma Fm Mwenyekiti wa mtaa wa Bwawani Bw.Sospeter Abeli amesema kuwa kinachosubiriwa hivi sasa ni mazungumzo baina ya viongozi wa mtaa na ofisi ya mkurugenzi.

Sauti ya Bw.Sospeter Abeli.

Aidha Mwenyekiti huyo amemaliza kwa kuwasihi wananchi kuendelea kuwa na subira huku mchakato wa kutatua changamoto hiyo ukiwa unaendelea.

Sauti ya Bw.Sospeter Abeli.