Dodoma FM
Dodoma FM
20 February 2026, 5:58 pm

Aidha ameongeza kuwa Hali hiyo inaweza kuchangia na kusahaulika Kwa majukumu ya kiulinzi na usalama na kupelekea kurejea Kwa matukio hayo.
Na Victor Chigwada.
Mkuu wa kituo Cha polisi Wilaya ya Mtumba kamanda OCD Issa Chau ameeleza Hali ya ulinzi na usalama katika Wilaya hiyo hususani Kata ya Ihumwa ambayo imekuwa na matukio ya wizi katika maduka na mifugo
Chau ameeleza kuwa miongoni mwa maeneo ambayo walifanikiwa kudhibiti wimbi la uhalifu ilikuwa ni ihumwa tofauti na Sasa inavyo ripotiwa
Aidha OCD Chau amesema kuwa IPO mipango ya kuhakikisha wanakomesha tabia hizo zinazo ibuka kwani wananchi wamekuwa na utayari wa kuunga mkono jitihada za ulinzi na usalama
Chau amesema kuwa wako tayari kufanya oparesheni za kutatua changamoto ya udozi na wizi wa Mali za wananchi Kwa kufuatilia hata uaminifu wa baadhi ya watumishi ikiwa ni pamoja na migambo wa doria