Dodoma FM

Airtel yazindua minara mitano mipya nchini

30 January 2026, 5:32 pm

Minara hiyo mipya imezinduliwa katika eneo  la kilindi Tanga, Mbalamaziwa – Njombe, Ruanda – Songea, Miombo – Sumbawanga, na Buhongwa – Mwanza.Picha na Airtel Tanzania.

Airtel Tanzania inaendelea kuipa kipaumbele upanuzi wa mtandao kama sehemu ya dhamira yake ya kukuza ujumuishi wa kidijitali, kuhakikisha wananchi wote nchini wanapata huduma za simu na intaneti zenye uhakika, gharama nafuu, na ubora wa juu.

Na Bennard Komba

Kampuni ya mawasiliano nchini AIRTEL TANZANIA imeendelea kujiweka karibu zaidi na wananchi baada ya kufanikiwa kuzindua minara mitano  mipya katika maeneo mbalimbali nchini.

Minara hiyo mipya imezinduliwa katika eneo  la kilindi Tanga, Mbalamaziwa – Njombe, Ruanda – Songea, Miombo – Sumbawanga, na Buhongwa – Mwanza, hatua inayolenga kuimarisha upatikanaji wa mtandao na kuboresha huduma za simu na intaneti kwa wananchi wanaoishi katika maeneo hayo

Mkazi wa Miombo, Sumbawanga ambaye ameshuhudia uzinduzi huo ameshukuru kampuni ya airtel Tanzania kwa kuzindua minara mipya huku akisema.

Douglas Mwingira ni Diwani wa Kata ya Ruanda mkoani Ruvuma ameishukuru Airtel kwa kuwekeza katika eneo hilo, akibainisha kuwa mnara huo utakuwa kichocheo cha maendeleo ya haraka.

Bi. Lydia Kalimunda ni Meneja wa Tawi la Airtel Tanga amesema mnara huo mpya utakuwa na mchango mkubwa katika kuwaunganisha wakazi na fursa zilizo nje ya maeneo yao ya karibu

Naye Bw. Malaki Mchala ni Meneja wa Kanda wa Airtel Mwanza wakati Tukio la uzinduzi likifanyika  Buhongwa ameleza athari chanya za mnara huo katika maisha ya kila siku na maendeleo ya wananchi

Sauti kina