Dodoma FM

Kata zatakiwa kutenga bajeti kwaajili ya kujenga masoko

06/03/2026, 16:25

Picha ni Mkuu wa mkoa wa Dodoma Mh. Rosemery Senyamule akiwa ametembelea banda la wakala wa Vipimo katika viwanja vya Nyerere Square jijini Dodoma.

Kliniki hiyo ya kutatua kero kwa wananchi itachukua takribani siku tatu na  Moja ya dhamira kuu ya serikali nikuhakikisha  mwananchi hatembei umbali mrefu kwenda kupata huduma badala yake wamezisogeza taasis zote za kiserikali katika eneo moja ili kutatua kero kwa wananchi.

Na Anwary Shaban.

Halmashauri ya jiji la Dodoma imeelekeza  kila kata kutenga kiasi cha shilingi milioni mia moja na hamsini  kujenga masoko kwa ajili ya wajasiriamali .

Hayo yamesemwa na mkuu wa wilaya ya Dodoma Alhaj Jabir Shekimweri  katika kliniki iliyo zikutanisha taasisi mbalimbali za kiserikali katika kutatua kero za wananchi mbalimbali ikiwa ni mafanikio ya siku 100 za Mhe.Dkt  Samia  Suluhu Hassan.

Sauti ya Alhaj Jabir Shekimweri 

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mh. Rosemery Senyamule  ameizungumzia cliniki iliyo zikutanisha taasis mbalimbalimbali za serikali kutatua kero za wananchi ambapo amesema wakazi wa Dodoma wanapaswa kuzitumia siku hizi zilizo tengwa kwaajili ya kutatuliwa kero zao.

Sauti ya Mh. Rosemery Senyamule 

Mh.Senyamule ameeleza kuwaa mpango wa utekelezaji wa kero za wananchi  ambayo inafahamika kwa  kauli mbiu isemayo Kero yako wajibu wangu  ilianza kutekelezwa tangu mwaka 2023 na bado unaendelea kufanyika  .

Sauti ya Mh. Rosemery Senyamule