Dodoma FM

Wananchi Mjelo kunufaika na mradi mpya wa maji

19 February 2026, 5:25 pm

Mradi huo utarahisisha huduma ya maji kijiji hapo.Picha na DUWASA.

Shirika la water mission tayari limeanza kusambaza mabomba ya maji katika vitongoji vya kijiji hicho.

Na Victor Chigwada.

Wakazi wa Kijiji cha Mjelo kata ya Handali Jijini Dodoma wamepata tumaini la kuondokana na adha ya maji baada ya shirika la water mission kusambaza mabomba ya maji katika vitongoji vya kijiji hicho.

Mwenyekiti wa Kijiji Cha Mjelo Bw.Emmanuel Tanaga ameeleza namna walivyo pokea mradi huo wa usambazaji maji kupitia shirika la water mission ambapo amesema mradi huo utarahisisha huduma ya maji kijiji hapo.

Sauti ya Bw.Emmanuel Tanaga.

Nao baadhi ya wakazi wa  Mjelo wamesema wanatamani kupata huduma ya maji nyumbani kwa kuvuta mabomba hayo ya maji kwani wameteseka muda mrefu kutembea umbali mrefu na kupanda foleni ili kupata huduma hiyo ya maji.

Sauti za wananchi.