Dodoma FM
Dodoma FM
25 March 2026, 16:43

Amekiri kusimama kwa ujenzi wa jengo la mama na mtoto ambalo limefikia kwenye hatua ya kupaua lakini ujenzi umekwama kwa sasa.
Na Victor Chigwada.
Wananchi wa vitongoji vya Ilolo na Muungano wilayani Chamwino wameiomba Serikali kuingilia kati ili ujenzi wa jengo la mama na mtoto uweze kuharakishwa ili kupunguza adha Kwa akina mama wajawazito
Wamesema kuwa kutokana na ujenzi wa jengo hilo kuchelewa kumepelea akina mama wajawazito kujifungulia kwenye wodi za wagonjwa wa kawaida jambo ambalo si salama kiafya.
Nae Mwenyekiti wa Kijiji hicho Bw.Matonya Mtukamsihi amekiri kusimama kwa ujenzi wa jengo la mama na mtoto ambalo limefikia kwenye hatua ya kupaua lakini ujenzi umekwama kwasasa.
Mtukamsihi ameongeza kuwa licha ya uwepo wa mikataba ya wadau wa madini mchanga lakini fedha hizo pia zinategemewa kwenye ujenzi wa sekondari na kupelekea kukwama kwa ujenzi wa jengo la mama na mtoto .