Dodoma FM
Dodoma FM
24 March 2026, 16:59

Mpango huo umepitishwa katika vijiji vya Lukole, Mzase, Kingiti, Iyenge, Kidenge, Mgoma, Nzogole na kitati ikiwa ni mwendelezo wa serikali kuhakikisha vijiji vyote nchini vinapangwa, kupimwa na kumilikishwa.
Na Steven Noel.
Wananchi wa vijiji nane vya Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa mkoani Dodoma wamepitisha mpango wa matumizi bora ya ardhi pamoja na sheria ndogo za kusimamia utekelezaji wake.
Mpango huo una lengo kupunguza migogoro ya ardhi kati ya wakulima, wafugaji na kudhibiti uvamizi wa maeneo na kupunguza uharibifu wa mazingira
Kazi ya kuandaa mpango wa matumizi bora ya ardhi kwa vijiji hivyo imefanywa na wananchi kwa kushirikiana wataalam wa Tume ya Taifa ya Mipango ya Matumizi ya Ardhi na wataalam kutoka Halmashauri ambapo baadhi ya wananchi wa vijiji hivyo wamesema mpango utawasaidia kulinda maeneo yao ya ardhi .

Baadhi ya Wananchi wa Kijiji cha mzase a wamesema mpango huo utasaidia kuchochea maendeleo Katika vijiji hivyo na kupunguza migogoro inayotokana na mwingiliano wa matumizi ya ardhi,
Nae Afisa ardhi kutoka tume ya MATUMIZI ya ardhi amesema kuwa mpango hu ni mkombozi wa mabadiliko ya tabia ya nchi na uhifadhi wa mazingira na katika kupata haki ya umiliki wa ardhi
Kwa upande wake makamu mwenyekiti wa halmashauri hiyo bwana Baraka Habari ameeleza umuhimu wa mpango huo kwa wananchi na serikali .