Dodoma FM

Wawekezaji  Nayu wasaidia kuboresha huduma za kijamii

20 January 2026, 6:03 pm

Misaada hiyo ya kijamii ambayo inatolewa na wawekezaji hao inawasaidia kuwapa wananchi matumaini ya kupiga hatua za kimaendeleo.Picha na Maelezo.

kumekuwa na ushirikiano wa karibu baina ya wawekezaji na wananchi hivyo imekuwa rahisi  wananchi kunufaika na misaada kutoka Kwa wawekezaji hao.

Na Victor Chigwada.

Wananchi wa Kijiji cha Nayu Kata ya Dabalo Wilayani Chamwino wametoa pongezi Kwa wawekezaji wa migodi ya dhahabu katika Kijiji Chao Kwa misaada ya kijamii wanayo itoa.

Wakizungumza na Taswira ya habari miongoni mwa wakazi hao wamesema misaada hiyo ya kijamii ambayo inatolewa na wawekezaji hao inawasaidia wananchi na kuwapa matumaini ya kupiga hatua za maendeleo.

Sauti za wananchi.

Mwenyekiti wa Kijiji Cha Nayu Bw.Samsoni Noha amesema kuwa kumekuwa na ushirikiano wa karibu baina ya wawekezaji na wananchi hivyo imekuwa rahisi  wananchi kunufaika na misaada kutoka Kwa wawekezaji hao.

Noha ameongeza kuwa kupitia uwekezaji wa sekta ya madini wamefanikiwa kutoa misaada ya chakula mashuleni sambamba na usimamizi wa ofisi za kijiji pamoja na ujenzi wa matundu ya vyoo .

Sauti ya Bw.Samsoni Noha