Dodoma FM

Vodacom kutoa kipaumbele kwa wenye mahitaji maalum

16 January 2026, 3:27 pm

Picha ni Afisa Mtendaji Mkuu wa Vodacom Tanzania PLC Philip Besiimire ( wa pili kushoto) akikata utepe kuashiria ufunguzi wa duka jipya la Vodacom jijini Dodoma. Picha na Fullshangwe Blog.

Besiimire amesema duka hilo ni mkombozi kwa wakazi wa Mkoa wa Dodoma na mikoa jirani iliyo katika Kanda ya Kati kutokana na kuboreshwa kwa huduma zake.

Na Yussuph Hassan.

Kampuni ya Mtandao wa Simu ya Vodacom imesema imejipanga kuhakikisha  inatoa huduma yenye kipaumbele kwa makundi  maalumu kwa kuwasimamia nakuwapa huduma bora sawa na wateja wengine.

Hayo yamesemwa na Mkuu wa kanda ya kati Vodacom Chiha Nchimbi na Msimamizi wa Maduka ya Vodacom Kanda ya Kati Bernard Kombe , wakati wa Uzinduzi wa Duka la Vodacom Jijini Dodoma  ambapo wamesema watahakikisha makundi ya watu wenye mahitaji maalumu  wanahudumiwa kwa wakati na kujali hali Zao.

Sauti ya Chiha Chimbi na Bernard Kombe.

Kwa upande wake Afisa Mtendaji Mkuu wa Mtandao wa Vodacom Tanzania, Philip Besiimire amesema watahakikisha wanaboresha Huduma na kukuza mawasiliano Maeneo mengi zaidi.

Sauti ya Philip Besiimire.