Dodoma FM

Wananchi waipongeza serikali ujio wa mradi wa maji Msanga

15 January 2026, 2:20 pm

Picha ni ujenzi wa mradi wa maji wa miji 28, wilaya ya Chamwino jijini Dodoma. Picha na DUWASA.

Wananchi hao wamefurahishwa na ujio wa mradi huo, huku wakiongeza kuwa mradi huo utawapunguzia umbali ambao walikuwa wakitembea kutafutamaji safi na salama.

Na Victor Chigwada.

Wananchi wa Kijiji cha Msanga Wilayani Chamwino wameipongeza Serikali Kwa ujenzi wa mradi mkubwa wa maji  kijijini hapo.

Wakiongea na taswira ya habari wanasema ujio wa mradi wa maji kijijini hapo utamaliza adha ya maji ambapo hapo awali walilazimika kutembea umbali mrefu kutafuta maji.

Sauti za wananchi.

Mwenyekiti wa Kijiji Cha Msanga Bw.Tibu Ally amesema  kukamilika Kwa mradi wa maji Kijiji hapo utasaidia kutibu changamoto ya maji katika vitongoji vingi vya Kijiji hicho

Sauti ya Hatibu Ally.