Dodoma FM

Mikopo ya 10% yawakwamua vijana kiuchumi

2 October 2025, 3:42 pm

Picha ni mmoja wa wanufaika wa mkopo wa 10% akiendelea na shughuli ya ushonaji. Picha na Dodoma FM.

Mikopo hiyo inawapa faida zaidi ikilinganishwa na mikopo mingine ya mtaani ambayo mara nyingi ina riba kubwa.

Na VictorChigwada.

Vijana wa Kata ya Msamalo, Wilaya ya Chamwino, wameipongeza serikali kwa kujali kundi la vijana, wanawake, na watu wenye ulemavu kwa kuendelea kutoa mikopo ya asilimia kumi.

Wakizungumza na Taswira ya Habari, baadhi ya vijana wamesema kuwa mikopo hiyo imekuwa ikisadia vijana wengi kuamka kifikra na kuanzisha miradi mbalimbali inayotoa ajira na kipato.

Wameongeza kuwa mikopo hiyo inawapa faida zaidi ikilinganishwa na mikopo mingine ya mtaani ambayo mara nyingi ina riba kubwa.

Sauti za vijana.

Aidha, wamewaomba vijana wenzao kujiunga katika vikundi mbalimbali ili kunufaika na mikopo hiyo, sambamba na kuhakikisha wanafanya marejeshokwa wakati sahihi ili wengine pia waweze kunufaika na mikopo isiyo na riba.

Sauti za vijana.

Kwa mujibu wa mwongozo wa Serikali, kila halmashauri inalazimika kutenga asilimia 10 ya mapato yake ya ndani kwa ajili ya mikopo isiyo na riba kwa vikundi vya wanawake (4%), vijana (4%), na watu wenye ulemavu (2%).