Dodoma FM

Uboreshaji wa zahanati wapunguza vifo Ihumwa

22 July 2025, 2:23 pm

wamepokea vifaa vilivowasaidia  vya kisasa ambavyo vimekua msaada mkubwa kwa wananchi.Picha na Lilian Leopold.

Ikumbukwe kuwa mradi wa ukarabati wa jengo la zahanati ya Ihumwa ulianza tarehe 10 /08/2023, ukigharimu kiasi cha shilingi milioni 235.9  fedha kutoka Shirika la Wahisani ABBOT.

Na Lilian Leopord.

Uboreshwaji  wa miundimbinu uliofanyika katika zahanati ya Ihumwa iliyopo jijini  Dodoma umesaidia wananchi kupata huduma bora na kupunguza  vifo vya akina mama wajawazito.

Picha ni Mganga Mfawidhi wa zahanati ya Ihumwa, Aisha Abubakari wakati akilezea uboreshwaji uliofanyika katika zahati hiyo.Picha na Lilian Leopord

Akizungumza  na Taswira ya habari Mganga Mfawidhi wa zahanati ya Ihumwa, Aisha Abubakari wakati akilezea uboreshwaji uliofanyika katika zahati hiyo amesema wapokea vifaa vilivowasaidia  vya kisasa ambavyo vimekua msaada mkubwa kwa wananchi.

Sauti ya Mganga mfawidhi.

Naye Berazel Kasuga ambaye ni Mkazi wa Ihumwa amesema uboreshaji wa zahanati hiyo umewasaidia wanawake na watoto ambao walikua wanapata changamoto ya kutembea za umbali mrefu kupata huduma za afya.

Sauti ya mwananchi.