Dodoma FM

Ukosefu wa vivuko reli ya SGR kilio kwa wakazi wa Mnase

20 May 2025, 3:53 pm

Hali hii inaleta changamoto kwa wanafunzi wanapo taka kuvuka kwenda shule pamoja na wananchi hasa wagonjwa wanapo vuka kwenda kupata huduma za Afya.Picha na Google.

Wananchi wanadai kuwa changamoto hii imeshindwa kupatiwa ufumbuzi.

Na Victor Chigwada.

Wananchi wa vitongoji vya malechela ,Lusinde na sokoine Kijiji Cha Mnase wameendelea kulia na changamoto ya kukosekana kivuko baina ya wananchi na reli ya mwendokasi(SGR)

Wakieleza namna changamoto hiyo ambavyo imekuwa ikiwaathili hususani watoto wadogo wanapo hitaji kuvuka kwenda shuleni pamoja na wajawazito na wagonjwa mbalimbali wanapo hitaji huduma za afya

Aidha wamesema kuwa changamoto hiyo ya kutokuwepo Kwa kivuko rasmi imekuwa ikipelekea kutumia njia za makalavati ya maji ili kuvuka eneo hilo jambo ambalo limewaathili wanafunzi hususani wa umri mdogo pindi wanapokutana na maji kwenye makaravati

Wakizungumza na taswira ya habari wameiomba Serikali kuingilia kati changamoto hiyo kwani mkandarasi wa mradi imekuwa ni muda mrefu ameshindwa kutelekeza ujenzi wa kivuko

Sauti za wananchi.

Ayubu Malima mwenyekiti kutoka vitongoji hivyo amekiri uwepo wa adha hiyo ambayo imeshindwa kupata suluhu tangu kuanza Kwa maradi wa ujenzi wa reli hata sasa

Sauti ya Ayubu Malima.