Dodoma FM

Wananchi kata ya Chamwino washiriki zoezi la usafi usafi

7 April 2025, 5:42 pm

Picha ni wananchi wa kata ya Chamwino Jijini Dodoma wakifanya usafi katika eneo la makaburi .Picha na Lilian Leopord.

Zoezi hilo ni enedelevu katika kata hiyo ambapo kila Jumamosi wananchi hujitokeza kwa ajili ya kufanya usafi katika maeneo mbalimbali ya kata hiyo.

Na Lilian Leopord.
Wananchi wa kata ya Chamwino jijini Dodoma wameshiriki katika zoezi la usafi wa mazingira katika maeneo mbalimbali ya kata hiyo.

Akizungumza Diwani wa kata ya Chamwino, Jumanne Ndege katika zoezi hilo, amewapongeza wananchi wa kata hiyo kwa kujitokeza kufanya usafi kwenye maeneo mbalimbali ikiwemo makaburi yaliyopo mkabala na shule ya Sekondari Hijra, lengo ikiwa ni kutekeleza ajenda ya kutunza na kulinda mazingira.

Sauti ya Jumanne Ndege.

Aidha Diwani Ngede amewataka viongozi wa mitaa kuwachukulia hatua kali za kisheria wale wate waliokaidi zoezi la kufanya usafi katika kata hiyo.

Picha ni mwenyekiti wa vikundi vya usafi akiongea na wananchi wa kata ya Chamwino.Picha na Lilian Leopord.
Sauti ya Jumanne Ndege.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Vikundi vya Usafi jiji la Dodoma amewataka wananchi kuzingatia suala la usafi hasa katika maeneo yanayowazunguka. Vilevile ametoa wito kwa wananchi kuhakikisha wanatunza taka vizuri na wanalipa hela kwa ajili ya taka hizo.

Sauti ya Mwenyekiti wa Vikundi vya Usafi.

Baadhi ya wananchi walioshiriki katika zoezi hilo akiwemo Amina Mgaya, Balozi wa Chinangali, Shina namba 2 na Mwanaasha Mohamed ambaye ni Mtendaji wa Mtaa wa Mwaja wameelezea jinsi wanavyoshiriki katika kuhakikisha kuwa wanaimarisha usafi wa mazingira.

Sauti za wananchi.