Dodoma FM

Wananchi watakiwa kuacha kujichukulia sheria mkononi

14 August 2024, 5:14 pm

Picha ni wananchi wakiwa wamejichukulia sheria mkononi.Picha na full shangwe blog.

Jeshi la Polisi liendelee kutoa Elimu kwa jamii kuhusu umuhimu wa jamii kufuata misingi ya sheria.

Na Seleman Kodima.
Baadhi ya Wananchi wamesema kitendo cha kujichukulia sheria mkononi ni hatua mbaya hivyo wanaliomba jeshi la Polisi kuendelea kutoa Elimu kwa jamii kuhusu umuhimu wa jamii kufuata misingi ya sheria katika matukio yote yanayohitaji haki.

Wakizungumza kwa Nyakati tofauti wakazi hao kutoka halmashauri ya jiji la Dodoma kuhusu uwepo wa matukio ya wananchi kujichukulia sheria mkononi nini kifanyike ili kupunguza vitendo hivyo.

Sauti za wananchi.

Hapo jana Jeshi la Polisi mkoa wa Dodoma limewataka Wananchi kuacha kujichukulia hatua mkononi badala yake watoe taarifa pindi wanapobaini kuna vitendo vyovyote vya uvunjifu wa amani.