Dodoma FM

Wanafunzi walalamika kukataliwa katika baadhi ya vyombo vya usafiri

19 July 2024, 6:27 pm

Picha ni mwanafunzi wa shule ya Sekondari akieleza changamoto wanazo pata katika usafiri . Picha na Nasma.

Licha ya kupanda na kushuka kwa bei ya nishati ya mafuta ya petroli Nchini kunakochangia ongezeko la bei za nauli katika vyombo vya usafiri ikiwemo daladala lakini mamlaka ya udhibiti wa usafiri wa ardhini LATRA haijabadili kiwango cha nauli kwa wanafunzi cha shilingi 200.

Na Mwandishi wetu.
Baadhi ya wanafunzi katika Jiji la Dodoma wamelalamikia usumbufu wanaoupata kutoka kwa wamiliki wa vyombo vya usafiri wakiwemo madereva wa daladala pindi wanapohitaji kupanda vyombo hivyo kuwahi shuleni nyakati za asubuhi na jioni watokapo masomoni.

Baadhi ya wanafunzi hao akiwemo alfa agrey pamoja na jailos ruben wamezungumza na Dodoma TV na kueleza kuwa changamoto ya kukataliwa katika baadhi ya vyombo vya usafiri imekuwepo kwa muda.
Wamesema hatua hiyo inawarudisha nyuma kitaaluma kutokana na kutumia muda mwingi kutafuta usafiri na wakati mwingine kuchelewa masomo darasani.

Sauti za Wanafunzi.
Picha ni daladala ambayo inapakia abiria katika kituo cha Soko la Machnga jijini Dodoma. Picha na Nasma.

Khamis ally ni moja ya dereva wa daladala katika jiji la Dodoma amezungumza na kituo hiki juu ya tuhuma hizo na kueleza kuwa utovu wa nidhamu kwa baadhi ya wanafunzi ni chanzo cha kubaguliwa katika vyombo hivyo.

Sauti ya Dereva wa daladala.

Sarah William mkazi wa kata ya mkonze Jijini Dodoma kama mzazi anasema hatua ya kukataliwa kwa waanfunzi katika vyombo vya usafiri inachangia hofu kwa wazazi juu ya usalama wa watoto wao.

Sauti ya Bi. Sara William