Dodoma FM

HakiElimu na wanafunzi wa mazingira magumu Mpwapwa

04/03/2026, 16:48

Picha ni Afisa Elimu kata ya Mazae Bi Honaratha Viane akiongea wakati wa kukabidhi bidhaa hizo.Picha na Steven Noel.

Msaada huo umetolewa kama chachu ya wanafunzi wenye mazingira magumu kutimiza ndoto zao za kimasomo.

Na Steven Noel.

Shirika la HakiElimu  limetoa  msaada wa sare za shule na vifaa  vingine vya kujifunzia kwa  wanafunzi  waishio katika mazingira magumu  wilayani Mpwapwa.

Akiongea wakati wa kukabidhi msaada huo Afisa Elimu kata ya Mazae Bi Honaratha Viane amesema msaada huo umetolewa ukawe chachu ya wanafunzi hao kutimiza ahadi zao za masomo .

Sauti ya Bi Honaratha Viane.