Dodoma FM

Serikali wilayani Mpwapwa yaingilia kati sakata la mtoto kupotea

26 January 2026, 5:11 pm

Wilaya ya Mpwapwa inakabiliwa na changamoto za wazazi au walezi kuwatoa watoto wao Kwenda mikoa ya mbali Kwa kazi za ndani  au kuchunga mifugo.Picha na Steven Noel.

Pamoja serikali kujitahidi kutoa Elimu kupitia vyombo mbalimbali lakin Bado wilaya ya Mpwapwa inakabiliwa na changamoto za wazazi au walezi kuwatoa watoto wao Kwenda mikoa ya mbali Kwa kazi za ndani  au kuchunga mifugo.

Na Steven Noel.

Hatimae serikali  wilaya Mpwapwa imeingilia kati sakata la mtoto  Rajabu Sulemani (13)wa Mpwapwa alieokotwa jijini Dar-es- salaam Katika mazingira magumu na kufanikisha kumrudisha Nyumbani na kukabidhiwa Kwa wazazi wake .

Akiongea na vyombo vya habari Afisa ustawi wilaya ya Mpwapwa Bi Rose Sichilima amesema kuwa kupitia mitandao ya kijamii  alipata taarifa za mtoto wa Mpwapwa  alitangazwa na vyombo vya clouds fm kuwa mtoto mdogo alieokotwa Polini  na mama msamalia ndipo ilipowalazimu kuchukua hatua za kilifuatilia suala Hilo Kwa kina na hatimae kufanikiwa kumrudisha kijana huyo  mikononi mwa wazazi wake.

Akiongea mama aliye muokota mtoto huyo Bi Mwamvita Mwanja amesema Katika shughuli zake alimuona mtoto huyo akiwa Porini amechoka na Yuko Katika Hali mbaya ya kiafya na kimuonekano na  ndioo alichukua jukumu la kuwapigia Simu clouds Ili wamtangaze Kwa lengo wapatikane wazazi wake.

Video 2. Bi Mwavita mwanja

Mama mzazi wa mtoto huyo Bi Asifiwe Ernest Alisema baada ya kutokea mgogoro wa kidamilia walitengana na mzazi mwenzie  huyo ndioo baba wa watoto aliwachukua watoto Kwa lengo la kukaa nao lakini nae aliwatoroka watoto na kukimbilia Tanga na kuwatelekeza watoto hao.

Kwa upande wake kaimu mkurugenzi mtendaji halmashauri ya Mpwapwa ambae pia ni Afisa maendeleo ya Jamii   bwana bwana Bahati Magumula alikemea tabia baadhi  ya wazazi kuwatumia watoto kama kitega uchumi na kuwakosesha Haki Yao ya kielimu.

Sauti ya kina.