Dodoma FM

Wakazi Nholi wataka uwazi wa mapato ya mgodi

8 January 2026, 4:46 pm

Licha ya kijiji kuingiza mapato bado hakuna taarifa rasmi wala vikao vilivyofanyika kueleza mapato hayo yalivyotumika. Picha na Nukta Habari.

Wameeleza kuwa uwazi wa mapato na matumizi yatokanayo na shughuli za uchimbaji wa madini katika mgodi wa Nholi ni jambo la msingi katika kuimarisha uwajibikaji na ushiriki wa wananchi katika masuala ya maendeleo ya kijiji.

Na Victor Chigwada.

Wakazi wa kijiji Cha Nholi wWilayani Chemba jijini Dodoma wameitaka serikali ya kijiji kuweka wazi mapato na matumizi yanayotokana na shughuli za uchimbaji wa madini katika mgodi wa Nholi kijijini hapo.

Wakizungumza na Taswira ya habari wananchi hao wamesema licha ya kijiji hicho kuingiza mapato kutokana na mgodi lakini wamekuwa na sintofahamu kwani hakuna vikao vyovyote vilivyofanyika kuhusu mapato na matumizi.

Sauti za wananchi.

Akijibu malalamiko ya wananchi mwenyekiti wa kijiji hicho Carolina Mtuli  amesema kuwa wanatarajia kuchukua hatua za ufuatiliaji kwani hapo awali kulikuwa  na taarifa za ucheleweshwaji wa asilimia za kijiji kutoka halmashauri.

Hivyo taarifa kamili ataitoa pindi atakapo kufanya ufuatiliaji kwa mtendaji wa kijiji .

Sauti ya Carolina Mtuli.